MALI

Mali yahitaji msaada zaidi wa kibinadamu

Mke wa rais wa Ufaransa bi Valerie Trierweiler amesema kuwa ameguswa sana na hali ya mambo nchini Mali baada ya kukamilisha ziara yake ya saa 48 katika taifa hilo lenye vita na koloni la kale la nchi yake. 

Mke wa rais wa Ufaransa  Valerie Trierwiler akiwa ziarani nchini Mali
Mke wa rais wa Ufaransa Valerie Trierwiler akiwa ziarani nchini Mali news24.com
Matangazo ya kibiashara

Mke huyo wa Rais Francois Hollande, ametembelea nchini Mali kama sehemu ya utume kwa ajili ya watoto na wanawake na alitembelea wagonjwa hospitalini na watoto wa shule, akielezea jukumu muhimu la askari wa kike katika kuleta amani.

Bi Valerie ameelza kuwa kamwe hatosahau ziara hiyo kutokana na kwamba amebaini ukubwa wa tatizo la Mali kinyume na inavyodhaniwa na akaongeza kuwa Mali inahitaji vitu vingi vya misaada ya kibinadamu.