AFRIKA KUSINI
Afya ya Mandela yaendelea kuimarika akiwa nyumbani
Rais wa zamani wa Afrika Kusini Nelson Mandela ameendelea kupata nafuu akiwa nyumbani kwake baada ya kukaa hospitalini kwa karibu miezi mitatu.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kwa mujibu wa mjukuu wake Mbuso Mandela amesema kuwa kwa sasa Mandela anaweza kukaa mwenyewe kwenye kitanda chake.
Mandela anaendelea kupatiwa uangalizi wa karibu wa afya yake akiwa nyumbani kwake mjini Johannesburg ambako alirejea baada ya kuruhusiwa kutoka hospitalini mnamo Septemba Mosi.
Mandela alikaa hospitalini mjini Pretoria kwa siku 86 huku afya yake ikitajwa kuwa mbaya lakini imara katika kipindi hicho chote.