MAREKANI-AFRIKA-Ushirikiano-Biashara

Marekani: Barack Obama ataka ushirikiano wa kina na bara la Afika

Serikali ya Marekani imewataka viongozi wa bara la Afrika kuheshimu tofauti za kisiasa zilizoko nchini mwao na kuwa na uvumilivu wa kisiasa ambao ndio nguzi kuu ya kuwa na demokrasia ya kweli katika kufikia mafanikio ya muda mrefu.

Rais wa Marekani, Barack Obama awataka viongozi Afrika kuwa makini na rasilimali ambazo China imekuwa ikizilenga kwenye bara la Afrika.
Rais wa Marekani, Barack Obama awataka viongozi Afrika kuwa makini na rasilimali ambazo China imekuwa ikizilenga kwenye bara la Afrika. REUTERS/Gary Cameron
Matangazo ya kibiashara

Wito huu umetolewa wakati wa ufunguzi wa mkutano kati ya viongozi hao na rais Barack Obama, ambaye alitumia siku ya kwanza ya mkutano huu, kusisitiza masuala ya usalama, biashara na demokrasia kama msingi mkuu utakaoshuhudia nchi za Afrika zikipata maendeleo ya haraka.

Kuhusu biashara, rais Obama amesema kuwa haoni shida nchi ya China kuwa mwekezaji mkubwa barani Afrika lakini akaonya kuhusu uwekezaji unaofanywa na taifa hilo na kuwataka viongozi hao kuwa makini na rasilimali ambazo China imekuwa ikizilenga kwenye bara hilo.

Rais wa Marekani, ambaye baba yake ni raia wa Kenya, hajatekeleza kile ambacho raia wa bara la Afrika walikua wanasubiri kutoka kwake.

Viongozi wa mataifa hamsini na Umoja wa Afrika wamealikwa. Hata hivo Jamhuri ya Afrika ya Kati, Zimbabwe, Soudani na Erythrea hazikupata mualiko. Rais wa Marekani anafanya mkutano huu ili kuanzisha uhusiano wa Marekani na bara nzima la Afrika.

Naibu mshauri wa masuala ya usalama na mawasiliano wa rais Barack Obama, Benjamin Rhodes, amesisitiza kile ambacho kilisemwa na rais Obama wakati wa ufunguzi wa mkutano huo.