ICC-KENYA-SHERIA-HAKI

Joyce Aluoch makamu mwenyekiti wa ICC

Nairobi, mji mkuu wa Kenya. Joyce Aluoch, raia wa Kenya amechaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa ICC.ambako Fidel Odinga, alikutwa amekufa.
Nairobi, mji mkuu wa Kenya. Joyce Aluoch, raia wa Kenya amechaguliwa kuwa makamu mwenyekiti wa ICC.ambako Fidel Odinga, alikutwa amekufa. AFP PHOTO / SIMON MAINA

Jaji Joyce Aluoch, ambaye ni raia wa Kenya amechaguliwa kama makamu mwenyekiti wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita ICC.

Matangazo ya kibiashara

Joyce Aluoch atahudumu kwenye wadhifa huo kwa kipindi cha miaka mitatu. Joyce Aluoch anashikilia wadhifa huo kufuatia uchaguzi uliyopigwa Jumatano wiki hii na majaji wa Mahakama ya Kimataifa ya Uhalifu wa Kivita.

Jaji Silvia Fernandez de Gurmendi kutoka Argentina amechaguliwa kuwa mwenyekiti wa ICC, naye jaji Kuniko Ozaki kutoka Japani, amechaguliwa kuwa makamu wa pili wa mwenyekiti wa ICC.

Mwenyekiti pamoja na wamakamu wake wawili wanaunda kile kinachojulikana kama bodi ya uwenyekiti wa Mahakama ya ICC, na bodi hiyo ndio hutoa mwongozo wa Mahakama kwa ujumla.

Mwenyekiti wa Mahakama ni mratibu wa Mahakama na vitengo vingine vilivyo chini ya mamlaka ya ICC.

Mwenyekiti wa Mahakama ya ICC ana madaraka kamili, bila kuingiliwa kwa kazi yake wala kushirikiana katika kazi yake na kiongozi wa Mashtaka.