Mjadala wa Wiki

Mustakabali wa Sudani Kusini matatani baada ya Machar kuondolewa serikalini

Imechapishwa:

Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amemuapisha Jenereli Taban Deng Gai kuwa Makamu wa kwanza wa rais kuchukua nafasi ya Riek Machar ambaye aliondoka jijini Juba mapema mwezi huu baada ya kuzuka kwa mapigano mapya.Hatua hii inadhirisha wazi mgawanyiko kati ya wanasiasa wa upinzani wa SPLM-IO wanaoongozwa na Machar ambaye hajulikani aliko.

Raisi Salva Kiir wa Sudani Kusini akimkumbatia makamu wake aliyemuapisha Taban Deng Gai
Raisi Salva Kiir wa Sudani Kusini akimkumbatia makamu wake aliyemuapisha Taban Deng Gai REUTERS/Jok Solomun
Vipindi vingine