NIGER-MALI

Niger yatangaza hali ya tahadhari kufuatia tishio la mashambulizi ya wanajihadi

Jeshi laimarisha ulinzi magharibi mwa Niger
Jeshi laimarisha ulinzi magharibi mwa Niger Wikipedia

Serikali ya Niger imetangaza hali ya tahadhari katika baadhi y amajimbo magharibi mwa maeneo yanayopakana na Mali baada ya mashambulizi kadhaa yanayodaiwa kutekelezwa na wanajihadi kutoka taifa jirani.

Matangazo ya kibiashara

Taarifa ya serikali kupitia televisheni ya taifa hilo imearifiwa kutekelezwa katika idara saba za kiserikali za mikoa ya Tillaberi na Tahoua.

Vikosi vya ulinzi na usalama vimepewa nguvu na mamlaka zaidi ikiwemo haki ya kupekua makazi ya watu wakati wowote,ilieleza taarifa hiyo.

Kwa mujibu wa serikali kujirudia kwa mashambulizi katika maeneo hayo kumehatarisha amani na kusababisha hofu miongoni mwa raia.

Maeneo yaliyoathirika ni "Ouallam, Ayorou, Bankilare, Abala na Banibangou katika mkoa wa Tillaberi na Tassara Tilia na Tahoua".