BENIN-SIASA-UCHAGUZI

Wananchi wa benin wasubiri matokeo ya uchaguzi wa rais

Wananchi wa Benin wanaendelea kusubiri kutangazwa kwa matokeo ya uchaguzi wa wabunge uliofanyika mwishoni mwa juma lililopita, uchaguzi ambao kwa mara ya kwanza umeshuhudia idadi ndogo ya wapiga kura waliojitokeza.

Wananchi wa Benin wakishiriki zoezi la kupiga kura
Wananchi wa Benin wakishiriki zoezi la kupiga kura RFI/Carine Frenk
Matangazo ya kibiashara

Wakati huu kukiwa hakuna muda maalumu wa kutangazwa kwa matokeo rasmi, taarifa kutoka ndani ya tume ya uchaguzi zinasema huenda yakaanza kutangazwa Alhamisi hii.

Upinzani nchini humo umeendelea kupinga mchakato wa uchaguzi ulivyokuwa na kutoa wito wa matokeo hayo kufutwa.

Uchaguzi wa Jumapili, umefanyika bila ya kuwepo kwa mgombea yeyote wa upinzani.