COTE D'IVOIRE-UCHAGUZI-SIASA-USALAMA

Uchaguzi Cote d'Ivoire: Outtara aongoza katika uchaguzi wa urais

Rais wa Cote d'Ivoire Alassane Ouattara anaongoza kwa mujibu wa matokeo ya awali ambayo yameanza kutangazwa nchini humo, baada ya wananchi wa taifa hilo mwishoni mwa wiki iliyopita, kushiriki katika uchgaguzi wa urais.

Rais Alassane Ouattara wakati wa mahojiano na vituo vya RFI na France 24, Jumanne, Oktoba 27, huko Abidjan.
Rais Alassane Ouattara wakati wa mahojiano na vituo vya RFI na France 24, Jumanne, Oktoba 27, huko Abidjan. RFI/France24
Matangazo ya kibiashara

Ouattara ambaye anaelekea kushinda katika uchaguzi huo uliosusiwa na wapinzani, amepata ushindi wa zaidi ya asimimia 90 Katika WIlaya ambazo kura zimeshahesabiwa.

Tayari chama cha rais huyo mwenye umri wa miaka 78, anayewania urais kwa muhula wa tatu, kimeonya kuwa hakitakuwa tayari kushiriki katika mazungumzo na wapinzani kuunda serikali ya mpito baada ya kususisa uchaguzi huo.

Msemaji wa upinzani nchini Cote d'Ivoire Pascal Affi N'Guessan wakati wa mkutano na waandishi wa habari huko Abidjan Novemba 1, 2020.
Msemaji wa upinzani nchini Cote d'Ivoire Pascal Affi N'Guessan wakati wa mkutano na waandishi wa habari huko Abidjan Novemba 1, 2020. RFI/Romain Ferré

Waangalizi wa ndani wamesema ni asilimlia 23 ya wapiga kura ndio walioshiriki katika zoezi hilo, baada ya wito wa upinzani kutaka wafausi wao kutoshiriki lakini pia baadhi ya barabara kufungwa na wapinzani wa rais Ouattara.

Wakati matokeo yanapoendelea kutangazwa, wagombea wa upinzani Henri Konan Bedie, na Pascal Affi N’Guessan wamedai kuwa watu zaidi ya 30 wameuawa katika machafuko ya kisiasa kuanzia Jumamosi iliyopita.