MAREKANI-CORONA-AFYA

Marekani yatoa dola bilioni 8.3 kwa kukabiliana na Virusi vya Covid-19

Huko Los Angeles, Wamarekani wanahifadhi maji, chakula na mahitaji menginz mengi kwa kukabiliana na virusi vya ugonjwa wa Covid-19 nchini Marekani, Februari 29, 2020.
Huko Los Angeles, Wamarekani wanahifadhi maji, chakula na mahitaji menginz mengi kwa kukabiliana na virusi vya ugonjwa wa Covid-19 nchini Marekani, Februari 29, 2020. Mark RALSTON / AFP

Baraza la Wawakilishi la Marekani limepitisha mpango wa dharura wa dola bilioni 8.3 ili kufadhili vita dhidi ya ugonjwa hatari wa Corona unaoendelea kusambaa nchini Marekani na mataifa mengine duniani.

Matangazo ya kibiashara

Bunge la Seneti limepitisha kwa kauli moja mpango huo wa dharura, wakati Marekani ikiendelea kupambana dhidi ya kuendea kwa virusi vya ugonjwa hatari vay Covid-19.

Rais Donald Trump alikuwa amependekeza bajeti ya kwanza ya dola bilioni 2,5, iliyochukuliwa na chama cha upinzani cha Democratic kuwa haitoshi kwa kukabiliana na kusambaa kwa virusi hivyo.

Mpango huo unakusudia kuboresha hatua ya mamlaka na kufadhili hasa utafiti na maendeleo ya chanjo, matibabu, na huduma za matibabu za mbali.