Mswada wa kuwasaidia Wamerekani walioathiriwa na Covid 19 wapitishwa
Imechapishwa:
Bunge la Congress nchini Marekani, limepitisha mswada wa Dola Trilioni 1 nukta 9 uliokuwa umependekezwa na rais Joe Biden, kuwasaidia Wamerekani ambao wameathiriwa zaidi na Janga la Covid 19.
Mswada huo uliungwa mkono na wawakilishi wote kutoka chama cha Democratic huku wale wa Republican wakiupinga.
Rais Biden sasa anatarajiwa kuutia saini siku ya Ijumaa, kwa ,mujibu wa msemaji wa Ikulu Jen Psaki.
Naweza kuwatibitishia kuwa rais atautia saini mswada huu siku ya Ijumaa katika Ikulu ya Marekani, tumekuwa tukipambana kwa siku kadhaa sasa kuhakikisha kuwa mswada huo unakamilika na sasa baada ya kupitishwa taratibu zingine zitafutwa na rais atakuwa tayari kuutia saini siku ya Ijumma.
Mswada huo unaeleza kuwa Wamarekani walio wengi walioathiriwa na mamabukizi ya Corona, watalipwa Dola 1,400.
Watu waliopoteza ajira kutokana na janga la Corona nchini humo, watalipwa Dola 300 hadi mwezi Septemba.
From $1,400 checks and unemployment relief to vaccines for every American — help is here. pic.twitter.com/R0AYaTbkTV
— The White House (@WhiteHouse) March 10, 2021
Aidha, imependekezwa kuwa mshahara wa chini kwa wafanyikazi nchini humo, kimeongezwa kutoka Dola 7.25 kwa saa moja hadi Dola 15.