BANGLADESH

Wakimbizi wa Rohingya wazuiwa kuhama maeneo nchini Bangladesh

Wakimbizi wa Rohinya Myanmar  katika mpango wa kuwatawanya 16 September 2017
Wakimbizi wa Rohinya Myanmar katika mpango wa kuwatawanya 16 September 2017 REUTERS/Mohammad Ponir Hossain

Bangladesh hapo jana imezuia kuhama kwa wakimbizi wa Rohingya, katika maeneo ambayo wamepangiwa na serikali hasa maeneo ya mpaka ambapo zaidi ya wakimbizi laki nne ambao wamekimbia vurugu nchini Myanmar wanaishi katika mazingira magumu.

Matangazo ya kibiashara

Hatua hizo ngumu zimechukuliwa wakati huu Dhaka ikijitahidi kukabiliana na kiwango cha mgogoro usio wa kawaida huku Waziri Mkuu wa Bangladesh Sheikh Hasina akijielekeza kwenye Mkutano Mkuu wa Umoja wa Mataifa kuomba msaada wa kimataifa.

 

Idadi ya wakimbizi wa Rohinya wanaokimbilia Bangladeshi  kutokana na mapigano nchini Myanmar imefika laki nne  (400,000).

 

Waziri mkuu huyo ameondoka siku moja baada ya serikali yake kumwita mjumbe wa Myanmar kwa mara ya tatu kupinga vitendo vinavyofanywa na nchi hiyo jirani yake.