URUSI-CORONA-AFYA

Coronavirus: Idadi ya maambukizi yapindukia 840,000 Urusi

Urusi imerekodi kesi mpya 5,482 za maambukizi ya virusi vya Corona leo Ijumaa, na kufanya jumla ya watu walioambukizwa virusi hivyo kufikia 839,981, idadi ambayo inaifanya nchi hiyo kuwa ya nne dunia iliyoathirika zaidi na ugnjwa huo.

Madaktari katika wodi ya matibabu ya wagonjwa wa Covid-19 katika hospitali ya Spasokukotsky huko Moscow, Aprili 22, 2020.
Madaktari katika wodi ya matibabu ya wagonjwa wa Covid-19 katika hospitali ya Spasokukotsky huko Moscow, Aprili 22, 2020. Yuri KADOBNOV / AFP
Matangazo ya kibiashara

Mamlaka nchini humo inasema watu 161 wamefariki dunia katika muda wa saa 24 zilizopita, na kufanya idadi ya vifo kufikia 13,963.

Hayo yanajiri wakati shirika la Afya Duniani, WHO, limesema kwamba kuongezeka kwa maambukizi ya virusi vya Corona katika nchi kadhaa kumesababishwa na vijana wapuuzi wasiojali kujikinga.

Mkurugenzi Mkuu wa shirika hilo Tedros Adhanom Ghebreyesus amewatadharisha vijana kwamba wao pia wanawezwa kuambukizwa.

Mpaka sasa watu milioni 17 wamekumbwa na maambukizi hayo duniani kote na 670,000 wameshakufa. Bwana Tedros amesisitiza kuwa vijana pia wanaweza kufa kutokana na maradhi ya Covid 19 na pia wanaweza kuwaambukiza watu wengine.