Besigye aondoka nchini Uganda
Kiongozi mkuu wa upinzani nchini Uganda Kizza Besigye ameitoroka nchi yake. Hayo ameyathibitisha mwenyewe kwenye mtandao wa twitter kuwa ameondoka nchini humo.
Imechapishwa:
Kwa mujibu wa Kizza Besigye akinukuliwa na gazeti la Daily Monitor Jumatatu wiki hii kuwa, aliamua kufuta safari yake kwenda nchini Afrika Kusini siku ya Jumanne kufuatia hatua ya polisi ya kuweka kizuizi nje ya nyumba yake.
Am now checked-in for my Nairobi flight. Police Offr this morning said I won't go anywhere. We fly & we shall overcome by defiance!! pic.twitter.com/N6NMYT0gLa
— Kifefe Kizza-Besigye (@kizzabesigye1) November 8, 2016
Serikali imekua ikijaribu kumzuia ili asiondoki bila mafanikio, amesema Bw. Besigye.
Hata hivyo msemaji wa polisi alikanusha madai hayo, akisema kuwa ni mbinu za Kizza Besigye kutaka kuonyesha kuwa hatendewi haki wakati sivyo.
Kizza Besigye anatarajiwa kuhutubia mkutano wa tume ya kimataifa ya mawakili mjini Johannesburg siku ya Alhamisi.