Habari RFI-Ki
Wimbi la wahubiri wafanyao miujiza tata ni uhuru wa kuabudu uliopitiliza?
Imechapishwa:
Cheza - 09:15
Nabii wa aina yake nchini Afrika kusini ametetea hatua yake ya kuwapulizia usoni dawa ya kuua wadudu wafuasi wanaofika kuombewa na kudai kuwa hatua hiyo huwaponya watu dhambi zao.Picha za muhubiri huyo Lethebo Rabalago zimesambaa katika mitandao ya kijamii,ameiambia tovuti moja kuwa wapo watu walioponywa kupitia dawa hiyo.Msikilizaji unazungumziaje wimbi la wahubiri wenye mbinu tata za maombezi na miujiza katika siku za hivi karibuni?Kwanini watu wanasaka miujiza?