Shambulio dhidi ya Mbowe: Marekani yaitaka Tanzania kuwakamata wahusika
Imechapishwa:
Siku moja baada ya kiongozi wa upinzani kutoka chama cha CHADEMA Freeman Mbowe kushambuliwa na watu wasiojulikana nymbani kwawke Dodoma, Marekani imetoa wito kwa serikali ya Tanzania kuanzisha uchunguzi haraka iwezekanavyo na kuwakamata wahusika.
Kwenye ukurasa wake wa Twitter Marekani kupitia ubalozi wake jijini Dar es Salaam, imelitaja shambulio la Freeman Mbowe miongoni mwa mlolongo mrefu wa matukio ya kusikitisha ya utumiaji wa nguvu na unyanyasaji yanayofanywa dhidi ya wanachama wa vyama vya upinzani.
Ubalozi wa Marekani umestushwa na kuhuzunishwa sana na tukio la kikatili la kushambuliwa kwa Mbunge na Mwenyekiti wa Chadema Freeman Mbowe hapo tarehe 9 Juni.
US Embassy Tanzania (@usembassytz) June 9, 2020
Tamko kamili https://t.co/BcXUTz3fEZ
Full statement https://t.co/pNtPz6RBYH#FreemanMbowe pic.twitter.com/PU0tBaMekt
Kiongozi mwingine wa upinzani kutoka chama hicho, Tundu Lissu alishambuliwa na kundi la watu wenye silaha alipokuwa amekaribia nyumbani kwake Dodoma tarehe 7 mwezi Septemba 2017. Lakini mpaka sasa uchunguzi kuhusu shambulio la mwanasiasa huyo haujazaa matunda yoyote.
Mapema wiki hii Tundu Lissu ambaye ni mkosoaji mkubwa wa utawala wa rais wa Tanzania John Magufuli alitangaza nia ya kuwania urais nchini humo wakati wa Uchaguzi Mkuu mwezi Oktoba.
Tundu Lissu kutoka chama Kikuu cha upinzani CHADEMA, kupitia mitandao ya kijamii ya chama chake alisema anaona anatosha kuleta mabadiliko nchini humo.
Lissu alisema anasubiri uamuzi wa chama chake ili kubaini iwapo atapambana na rais Magufuli.
Anaishi nchini Ubelgiji, alikoenda mwaka 2017 kutibiwa baada ya kupigwa risasi na watu wasiojulikana jiji Dodoma, na licha ya kusema kuwa amepona hajarudi nyumbani kwa kile anachokieleza ni kwa sababu za kiusalama.