Madakati wanaendelea na mgomo wao kwa siku ya pili nchini Kenya
Madaktari wanaofanya kazi kwenye hospital za umma nchini Kenya, kwa siku ya pili leo, wanaendelea na mgomo wao kulalamikia kutopewa bima ya afya na ukosefu wa vifaa vya kujikinga wanapowatibu wagonjwa wa janga la COVID-19.
Imechapishwa:
Mgomo huu unakuja wakati huu nchi nchi hiyo inapoendelea kukabiliana na janga la Corona.
Serikali ya Kenya kupitia Waziri wa afya Mutahi Kagwe imetishia kuwafuta kazi madaktari na wahudumu walioamua kugoma.
Kufikia sasa Kenya imerekodi visa 94,614 vya maambukizi ya virusi vya Corona baada ya visa vipya 114 kuthibitishwa na vifo 1,644 baada ya watu wengine 5 kuthibitishwa kufariki dunia kutoka na janga hilo hatari la COVID-19.
Watu 325 wameripotiwa kupona virusi hivyo na kufanya idadi ya jumla ya watu waliopona kufikia 76,060.