SYRIA-USALAMA

Mapiganao yaendelea kurindima katika mji wa Allepo

Jeshi la Syria na wapiganaji wa upinzani wameendelea kupambana katika mji wa Allepo na kusababisha vifo vya watu 41 kwa muda wa siku tatu zilizopita.

Vikosi vya usalama vya Syria vikiwaokoa wafanyakazi wa hopitali ya Muhafaza Aleppo, baada ya waasi kurusha risasi, Mei 3 2016.
Vikosi vya usalama vya Syria vikiwaokoa wafanyakazi wa hopitali ya Muhafaza Aleppo, baada ya waasi kurusha risasi, Mei 3 2016. GEORGE OURFALIAN / AFP
Matangazo ya kibiashara

Wanaharakati wa haki za Binadamu wanasema miongoni mwa watu waliopoteza maisha ni watoto 17.

Wakati makabiliano hayo yakiendelea, serikali ya Syria imewashtumu waasi wa kwa kurusha mabomu yenye gesi katika ngome ya wanajeshi wake.

Staffan de Mistura Msuluhishi Mkuu wa mzozo huu amelaani mashambulizi hayo anayosema wanawauawa raia wasiokuwa na hatia.