AFGHANISTAN-USALAMA
Kumi na nane wauawa katika shambulio la Kabul
Takriban watu 18 wameuawa katika shambulio la kujitoa muhanga dhidi ya kituo cha elimu huko Kabul, shamvulio lililotokea siku ya Jumamosi, vyanzo vya usalama kutoka Afghanistan vimebaini.
Imechapishwa:
Matangazo ya kibiashara
Kulingana na Wizara ya Mambo ya Ndani, maiti kumi na tatu zimepatikana na watu 57 wamejeruhiwa katika shambulio hilo.
Kulingana na msemaji wa wizara hiyo, mhalifu huyo alilipua vilipuzi katika mtaa ulio karibu na kituo cha elimu cha Denmark.
Kundi la Islamic State, katika taarifa, limekiri kuhusika na shambulio hilo.
Msemaji wa Taliban amekanusha kuhusika kwa shambulio hilo.