Bomu feki lazua kizaaza Old Trafford
Imechapishwa:
Watazamaji 75600 walitakiwa kuondoka Jumapili hii iliyopita katika uwanja wa Old Trafford, wakati walipokua wakijiandaa kutazama mchuano kati ya Machester United na Bournemouth.
Uamzi huo ulichukuliwa na polisi baada ya kugundua kifaa kilichofananishwa na bomu. Mara moja mchuano ulikua unatazamiwa klupigwa ulifutwa na kuahirishwa hadi Jumanne Mei 17 2;00 usiku.
Kifaa hicho kiliachwa katika uwanja huo na kampuni moja ya ulinzi iliyokuwa ikifanya mazoezi na mbwa wa kunusa vilipuzi siku nne zilizopita. Ugunduzi huo ulisababisha mechi ya mwisho ya ligi kuu msimu huu katika uwanja huo wa Manchester United kuahirishwa na mashabiki kuamriwa kuondoka.
Polisi jiji la Manchester katika akaunti yake ya Twitter immesema kuwa kifaa kilichopatikana katika uwanja wa Old Trafford, hakikuwa bomu bali kilikuwa kifaa cha mafunzo ya vilipuzi.
Suspicious item found at Old Trafford today, which required controlled explosion, was a training device https://t.co/55n06zNwU3
— G M Police (@gmpolice) May 15, 2016
Bomb disposal experts carried out controlled explosion at Old Trafford on what is described as incredibly lifelike explosive device...
— G M Police (@gmpolice) May 15, 2016
Latest update: A controlled explosion has just been carried out within the stadium by bomb disposal experts at Old Trafford. More to follow.
— G M Police (@gmpolice) May 15, 2016