EVERTON-SOKA-GOR MAHIA

Everton kuchuana na Gor Mahia mwezi Novemba

Kikosi cha Everton kilichotembelea Tanzania mwaka 2017 ambapo kilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Gor Mahia
Kikosi cha Everton kilichotembelea Tanzania mwaka 2017 ambapo kilicheza mechi ya kirafiki dhidi ya Gor Mahia The Citizen

Everton ya Uingereza itaipokea Gor Mahia katika mchuano wa Sports Pesa utakaochezwa mwezi Novemba katika Uwanja w a Goodson Park.

Matangazo ya kibiashara

Mchezo huo utakuwa maalumu kwa kuwa nia taji la Sports Pesa. Gor Mahia ilipata nafasi ya kuchuana na Everton baada ya kuishinda Simba SC ya Tanzania kwa mabao 2-0.

Awali, mchezo huo ulipangwa kuchezwa mwezi Julai lakini umesogezwa mbele kutokana na sababu mbalimbali.

Everton na Gor Mahia zote zinadhaminiwa na kampuni ya Sports Pesa.