UGIRIKI-UCHUMI

Ugiriki kupata afueni katika uchumi wake

Waziri Mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras mbele ya Wabunge.
Waziri Mkuu wa Ugiriki Alexis Tsipras mbele ya Wabunge. REUTERS/Alkis Konstantinidis

Bunge nchini Ugiriki limefanya mageuzi ya sheria ya kodi na mafao muda mfupi kabla ya kuanza kwa mkutano muhimu hii leo utakaowakutanisha mawaziri wa fedha kutoka mataifa yanayotumia sarafu ya Euro.

Matangazo ya kibiashara

Hatua hizo tata zinaweza kufungua fursa zaidi ya kimataifa kwa taifa hilo kupata fedha na kuruhusu kukopesheka kwa awamu mkopo wa kiasi cha yuro bilioni 4.

Kabla ya kura hiyo, waandamanaji jijini Athens walishambulia polisi kwa kutumia mabomu ya petroli ,polisi ambao waliwasambaratisha kwa kutumia mabomu ya machozi.

Vyama vya wafanyakazi vinasema nchi hiyo haiwezi kuvumilia mzunguko mwingine mkali wa kubana matumizi.