Hillary Clinton ashindwa kumuangusha Bernie Sanders
Imechapishwa: Imehaririwa:
Baada ya kampeni ngumu, mgombea urais wa chama cha Democratic Hillary Clinton amedai ushindi mdogo Jumanne hii katika jimbo la Kentucky katika kura za mchujo. Lakini Bernie Sanders, ambaye ameibuka mshindi katika jimbo la Oregon, ameahidi kubaki katika mbio za urais katika chama cha Democratic hadi mwisho.
Afisa anayesimamia uchaguzi katika jimbo la Kentucky, Alison Lundergan Grimes, ametangaza kwenye runinga ya CNN kwamba Hillary Clinton ameshinda uchaguzi katika jimbo hilo.
"Tumeshinda uchaguzi katika jimbo la Kentucky!" Hillary Clinton ameandika kwenye akaunti yake ya Twitter.
We just won Kentucky! Thanks to everyone who turned out. We’re always stronger united. https://t.co/8qYPHIje8I pic.twitter.com/elNUP4nFoO
— Hillary Clinton (@HillaryClinton) May 18, 2016
Kwa mujibu wa matokeo kwa jumla ya 99.9% ya vituo vya kupigia kura, Hillary Clinton amepata 46.8% ya kura dhidi ya 46.3% ya kura alizopata Seneta kutoka Vermont, sawa na chini ya kura 2,000 kwa jumla ya zaidi ya kura 450,000.
Lakini Bernie Sanders amemshinda kirahisi Waziri wa zamani wa Mambo ya Nje wa Marekanii, katika jimbo la Oregon, katika pwani ya Pasifiki, kwa 53% ya kura kwa mujibu wa matokeo ya awali.
Chama cha Republican kimeendesha zoezi la uchaguzi wa mchujo katika jimbo la Oregon pekee. Donald Trump, mgombea pekee katika mbio hizo, ingawa majina ya washindani wake wa zamani yamebakia kwenye kadi za kura.